Wednesday, November 16, 2016

Agizo la Serikali kwa wanafunzi waliohitimu kidato cha sita

Agizo la Serikali kwa wanafunzi waliohitimu kidato cha sita mwezi Mei mwaka huu Ambao Hawakujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)

Serikali amewaagiza wote waliohitimu kidato cha sita Mei mwaka huu na ambao hawajajiunga na vyuo vya elimu ya juu, wakaripoti katika kambi za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Desemba Mosi, mwaka huu.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi ametoa agizo hilo mjini Dodoma alipozungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Habari wa Bunge.

Dk Mwinyi alisema Mei na Juni mwaka huu, JKT iliwafanyia usaili vijana wa kujiunga na JKT kwa kujitolea. Alisema usaili huo ulifanyika kwa kushirikiana na kamati za ulinzi za wilaya na mikoa.

“Wizara ya Ulinzi na JKT inapenda kuwatangazia vijana wote waliosailiwa Juni mwaka huu, kujiunga na JKT kwa kujitolea, waripoti kwenye kambi walizopangiwa ifikapo Desemba Mosi mwaka huu kwa nauli zao,” amesema Dk Mwinyi.

Dk Mwinyi amesema mafunzo hayo ni ya miezi mitatu kwa mafunzo yenye utaratibu wa kawaida na miaka miwili kwa wa kujitolea.

Ili kufanikisha hilo, Wizara ilimuagiza Mkuu wa JKT kufufua kambi ya Makuyuni JKT iwe miongoni mwa kambi kuanzia Desemba mwaka huu.

Aliagiza kambi za Luwa na Milundikwa za mkoani Rukwa, zirejeshwe kwa shughuli za JKT za kilimo na ufugaji.

Dk Mwinyi alimuagiza Mkuu huyo wa JKT pia kambi ya Mpwapwa irejeshwe kwa ajili ya kuendesha mafunzo ya kilimo na ufugaji ndani ya JKT.

Orodha ya vyuo 26 vilivyofutiwa usajili na NACTE



Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limevifungia vyuo vya ufundi 26 kutokana na makosa mbalimbali, ikiwamo kushindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa katika cheti cha usajili wa vyuo hivyo, huku likisimamsisha utoaji wa programu zilizokuwa zikitolewa katika vyuo 20 ambazo hazijasajiliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Kaimu Katibu mtendaji wa NACTE, Dkt. Adolf Rutayuga, alisema kuwa wamekuwa wakifuatilia vyuo vya ufundi ili kutathmini kama vinafuata viwango vya ubora wa kitaaluma vilivyowekwa na NACTE katika kutoa mafunzo.
 
Katibu huyo amesema kuwa baada ya kufanya uchunguzi huo, wamebaini vyuo 26 vilishindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na NACTE katika cheti cha usajili, huku vyuo 20 vikitoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa chini ya idara isiyotambulika,wakati vyuo viwili vikiwa na vituo vya satellite/Kampasi ambavyo navyo havijathibitishwa na chombo husika.

NACTE ni bodi iliyoanzishwa kisheria chini ya Sheria ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi, kifungu cha 129, kusimamia na kuratibu utoaji wa elimu ya ufundi na mafunzo nchini Tanzania.  Chini ya sheria hiyo, ili kufikia na kudumisha hali ya mtoa mafunzo, vyuo vyote vinatakiwa viwe vimesajiliwa, vibali na kuwa mitaala iliyopitishwa na baraza. Vyuo haviruhusiwi kuanza kutoa kuanza kutoa huduma yoyote ya mafunzo bila idhini ya baraza.
 
Hapa chini ni mgwanyo wa vyuo katika makundi matatu na hatua zilizochokuliwa dhidi ya kila kundi
 
                    Vyuo vya Ufundi vilivyofutiwa usajili
S/NCHUO
1Institute of Management and Development Studies – Iringa
2Green Hill Institute – Mbeya
3Institute of Business and Social Studies – Mbeya
4Loyal College of Africa – Mbeya
5Mbeya Training College – Mbeya
6Mbengwenya College of Business and Information Technology –Mbinga
7New Focus College – Mbeya
8Shukrani International College of Business and Administration –  Mbeya
9Majority Teachers College – Mbeya
10Rukwa College of Health Sciences – Sumbawanga
11MAM Institute of Education – Mbeya
12Belvedere Business and Technology College – Mwanza
13Geita Medical Laboratory Sciences and Nursing Training College – Geita
14Global Community College – Geita
15Muleba Academy Institute – Muleba
16St. Bernard Health Training Institute – Katoro, Geita
17Victoria Institute of Tourism and Hotel Management – Mwanza
18Gisan Institute of Health Sciences – Mwanza
19Dar es Salaam Institute of Business Management – Dar es Salaam
20SAMFELIS College of Business Studies – Dar es Salaam
21Ellys Institute of Technology – Bunda, Mara
22Tanzania Institute of Chartered Secretaries and Administrators – Arusha
23Emmanuel Community College – Kibaha
24Modern Commercial Institute – Dar es Salaam
25Marian College of Law – Dar es Salaam
 Vyuo vya Ufundi vinavyotoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa
S/NCHUOMAFUNZO
1MISO Teachers College – MafingaCompetence Building Network (CBN) – a Certificate in Early Childhood Education
2Tusaale Teachers College – MafingaCompetence Building Network (CBN) – a Certificate in Early Childhood Education
3The St. Joseph’s College Institute of Business and Management (SJCIBM) – Morogoro
4The Golden Training Institute – Dar es Salaam
5Nkrumah Mkoka Teachers College – Kongwa, Dodoma
6National Institute of Agriculture (Chuo cha Kilimo cha Taifa) – Arusha
7Musoma Utalii Training College – Musoma
8Mwanza Polytechnic Institute – Mwanza
9Mwanza Polytechnic Institute – Maswa
10Ruter Institute of Financial Management – Mwanza
11Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Mwanza
12Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Geita
13Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Bukoba
14Singni International Training Institute – Bukoba
15Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Kahama
16Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Simiyu
17Richrise Teachers College – Geita
18Twiga Training Institute – Musoma
19Zoom Polytechnic Institute – Bukoba
20St. Thomas Training College – Shinyanga
Jedwali 3: Vyuo vya Ufundi vyenye Vituo vya Satellite / Kampasi
S/NCHUO
1MISO Teachers College – Mafinga
2Rungemba Teachers College – Mafinga

TCU-PUBLIC NOTICE


Procedures for Inter-University Transfers in 2016/2017 Academic Year

The past experience has shown that management of inter-university transfers
has been a challenging and time consuming task. For example, in the last
academic year, approximately 3,000 transfers were processed, approved
and submitted to HESLB for loan re-allocation. Based on observed challenges,
the Commission has reviewed the modality of handling transfers of First Year
students as follows:
(a) Applications for transfers should be submitted in writing to the institution
to which a student wants to transfer to;

(b) The transfer applications must comply with the following criteria;
i. The student to be transferred must have been previously
selected into one of the degree programmes;

ii. The programme to which transfer is sought must have empty
slots to accommodate new students

iii. The applicant must possess the minimum entry requirements
for that particular degree programme

iv. The applicant’s admission entry points to the programme
he/she to be admitted should either be equal or above the
cut -off point to the programme for which transfer is sought.

(c) Receiving institutions should approve the transfer in writing and submit
to TCU for validation and documentation;

(d) The list of transferred students from receiving institutions should be
submitted to TCU by 18th November 2016;

(e) All transfers which do not meet the criteria stipulated in part (b) shall be
nullified by TCU;

(f) Transfers submitted to TCU after the deadline will not be endorsed;

(g) The list of endorsed transfers shall be published into TCU website;

(h) All transfers endorsed by the Commission will be submitted to HESLB by
30th November 2016 for their appropriate action.

The Executive Secretary
Tanzania Commission for Universities

Kubainika kwa Wanafunzi Waliowasilisha Vyeti Feki Vya Vifo Vya Wazazi Wao HESLB

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) imebaini kuwepo kwa baadhi ya wanafunzi ambao wamewasilisha vyeti feki vya vifo vya wazazi wao ili waonekane kama ni watoto yatima; hivyo wapewe kipaumbele cha kupatiwa mkopo. 

Kuwepo kwa vyeti hivyo vya bandia kumegunduliwa na bodi hiyo baada ya kupeleka nakala za vyeti vyote vya vifo ofisi ya Msajili wa Vizazi na Vifo (Rita) kwa ajili ya uthibitisho ndipo ikagundulika kuwepo kwa kasoro hizo.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul- Razaq Badru, amesema  kuwa wahusika wote ambao wamewasilisha vyeti hivyo feki suala lao limekabidhiwa kwa mamlaka zinazoshughulika na makosa ya jinai.

Hata hivyo, Badru hakutaka kuingia kwa undani kuhusu suala hilo kwa maelezo kuwa bado wanaendelea na ukaguzi.

“Bado tunaendelea kuchunguza na idadi yao hapa sina, tukikamilisha tutawaita kuwaambia idadi yao,” alisema Badru na kuongeza kuwa kutokana na kasoro hizo, ndio maana kuna baadhi ya watu wanaolalamika kuwa ni yatima, lakini hawakupata mkopo. 

“Hayo malalamiko ya kwamba kuna yatima wamekosa mikopo tumeyasikia, lakini na sisi tunajiridhisha kuwa huyu ni yatima baada ya kupata uthibitisho wa vyeti vya vifo kutoka Rita,” alisema Badru.

Aliongeza kuwa hata wale ambao ni wanafunzi wenye ulemavu, bodi hiyo haiwezi kuwaamini kama ni walemavu, bali hadi wapate uthibitisho kutoka kwa daktari wa wilaya (DMO) kuthibitisha ulemavu wa mwombaji.

Alisema baadhi ya wanafunzi ambao wanalalamika kuwa wamekosa mikopo ni wale ambao maombi yao yalikaguliwa na kukutwa na dosari kadhaa, na wakaombwa wazirekebishe kasoro hizo, lakini baadhi yao hawakufanya hivyo.

Badru alisema bodi yake baada ya kuchambua maombi ya waombaji wote; hadi sasa imeshatoa mikopo kwa wanafunzi wote wanaostahili wakiwemo yatima, walemavu, wanafunzi wanaosoma kozi za kipaumbele na wahitaji wanaosoma kozi zingine.

Akizungumzia suala la baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) ambao wamekosa mikopo na kulazimika kurudi makwao, Badru alisema wanafunzi hao yawezekana ni miongoni mwa wale ambao hawakukidhi vigezo vya kuweza kupewa mkopo.

“Pale Dodoma tumetoa mkopo kwa wanafunzi wapya takribani 3,000, hivyo hao wanaoondoka kurudi nyumbani yawezekana wako kwenye kundi la wanafunzi ambao hawakukidhi vigezo vya kupewa mkopo,” alisema Badru.

Alisema sio rahisi kutoa mkopo kwa wanafunzi wote, kwani Serikal inaendeshwa kwa bajeti na mwaka huu wamechagua kusomesha wanafunzi 25,000 kulingana na bajeti iliyopo pamoja na kulingana na mahitaji ya wataalamu wanaotakiwa na kutokana na vipaumbele vyake.

Alisema anatambua kuna wanafunzi zaidi ya 10,000 ambao wamekosa mikopo na kuongeza; “lakini bajeti ya mwaka huu imeishia hapo, mwaka kesho tunaweza kuishauri Serikali iongeze fedha baada ya kuwa tumefanya tathmini uhitaji wa mikopo hiyo.”

Hata hivyo, Badru alisema kuna wanafunzi ambao wanasoma kozi za kipaumbele, lakini wazazi wao wana uwezo, hao nao hawakupatiwa mikopo licha ya kuwa kwenye kundi la wanaostahili mkopo.

“Kuna mtu anasomea udaktari, lakini wazazi wake wana uwezo, na kuna mwanafunzi anasomea sayansi ya jamii na wazazi wake ni watu wasio na uwezo, hapo lazima tuangalie mhitaji ni yupi kati ya hao wawili na ndiye tunampatia mkopo,” alisema Badru.

Alisema kuna wanafunzi wanasoma kozi za kipaumbele baadhi yao hawakupata mkopo kabisa na baadhi yao wamepatiwa mkopo kidogo baada ya bodi hiyo kufanya tathmini ya hali ya uchumi ya wazazi au walezi wa mwombaji.

Mwigulu aagiza Wahamiaji Haramu Warudishwe Nchini Kwao


Serikali imeagiza idara ya uhamiaji nchini kufanya uhakiki upya wa vibali vya wahamiaji wote walioko nchini na kwa wale ambao hawana sifa zinazostahili warudishwe kwenye nchi zao kwakuwa wanaishi nchini kinyume na sheria za nchi zinavyoelekeza.

Agizo hilo limetolewa jana na waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mhe. Mwigulu Nchemba alipokutana na viongozi wa idara ya uhamiaji nchini kwaajili ya kujadili na kutatua kero mbalimbali katika idara hiyo.

Kwa upande wa mifumo ya utoaji vibali Mhe. Mwigulu ameiagiza idara hiyo iunde tume maalum ya kujadili nakuangalia namna ya kuweka mifumo maalum ya kutoa vibali vya uraia kwa urahisi ili kupunguza malalamiko na ufisadi ambao kama hautatatuliwa mapema utasababisha hasara kwa taifa.

Aidha aliwaagiza watawala katika idara hiyo kutenda haki kwa watumishi wake na watanzania kwa ujumla sambamba na kuwalipa madeni yao watumishi wapya walioajiriwa na idara ya uamiaji nchini.

ORODHA YA WADAIWA SUGU WA MIKOPO VYUO VIKUU HII HAPA

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inatangaza orodha ya majina ya Wadaiwa Sugu ambao wamehitimu katika Vyuo mbalimbali vya Elimu ya Juu kuanzia mwaka wa masomo 1994/1995. Wasugu hao wanapewa siku 30 kulipa madeni yao ndani ya muda huo kabla hatua za kisheria hazijachukuliwa na wahusika kulazimika kulipia gharama za kuwasaka na kuendesha kesi.
Kwa mawasiliano zaidi piga 0763 459 165 au 0767 513 208 au tembelea ofisi zetu za Makao Makuu, Dar es salaam au ofisi zetu za kanda zilizopo Dodoma, Zanzibar, Mwanza na Arusha.
Kuona orodha hiyo tembelea
http://olas.heslb.go.tz/index.php/defaulters