Tuesday, October 18, 2016

MAJINA YA MIKOPO VYUO VIKUU 2016/2017

MAJINA YA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU WALIOPATA MKOPO 2016/2017

MUONGOZO WA UTOAJI MIKOPO

JUMUIA YA WANAFUNZI WA TAASISI ZA ELIMU YA JUU TANZANIA (TAHLISO)
                                                      IMG-20160330-WA0041
                    TAARIFA KWA WANAFUNZI WA TAASISI ZA ELIMU YA JUU

YAH: MUONGOZO WA UTOAJI MIKOPO ULIOTOLEWA NA WIZARA YA ELIMU ,   
                                        SAYANSI NA TEKINOLOJIA.
Jumuia ya Wanafunzi wa  Taasisi za Elimu ya juu Tanzania (TAHLISO) inawataarifu wanafunzi wote wa vyuo vikuu namna ilivyoshughulikia na kupata utatuzi wa Muongozo uliotolewa na Wizara kama ifuatavyo.
Waraka uliotolewa na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Tarehe 14/10/2016 ulitoa ufafanuzi namna mkopo utakavyotolewa kwa mwaka huu 2016/2017 kwa wanafunzi wapya wanaojiunga na masomo kwa mwaka huu “kuanzia mwaka huu wa masomo ,wanufaikawote wa mikopo (wapya na wanaoendelea na masomo)watakopeshwa kulingana na uwezo wao (means tested) katika vipengele vyote vya mkopo” Kufuatia maelezo hayo ni dhahiri mikopo kwa wanafunzi wanaoendele hasa kwa wale wenye wazazi  bila kujali anauwezo ama hana uwezo mikopo yao ingepungua kutoka kwenye asilimia walizopangiwa awali, hata hivyo kwa muongozo huo ungepelekea fedha inayotolewa kwa ajili ya chakula na malazi (boom) kupungua jambo ambalo lingepelekea wanafunzi wengi kushindwa kuendelea na masomo kutokana na uwezo wa familia wanazotoka hasa watoto wa maskini ambao hutegemea fedha hizohizo za boom kulipia sehemu ya ada iliyobakia na huku wakiendelea kuishi maisha ya shida vyuoni.
TAHLISO ambayo ndio chombo cha kutetea maslahi ya wanafunzi wote wa vyuo vikuu  tumeliingilia kati swala hilo kwa kufanya mazungumzo na uongozi wa bodi ya mikopo  HESLB  pamoja na mh.Waziri wa Elimu ,Sayansi na Teknolojia Prof.Ndalichako juu ya kubadili msimamo wa muongozo huo kwakua utawaathiri wanafunzi wengi ambao ni watoto wa maskini.
Katika majadiliano yetu yaliongozwa na hoja mbili zinazohusu wadahiliwa wapya na wanaoendelea na masomo, tumekubalina yafuatayo:
1.      Muongozo mpya wa utoaji mikopo uliotolewa kwa mwaka huu wa masomo 206/2017 utawahusu wadahiliwa wapya wanaoanza masomo.
2.      Wanafunzi wanaonufaika na mikopo wanaoendelea na masomo wao wataendelea na utaratibu kama ulivyokuwa tangu awali walivyoingia makubaliano na utaratibu mpya hautawaathiri.
Hata hivyo zoezi la serikali la kuhakikisha kwamba kila mwanafunzi mnufaika anayestahili kupata mkopo anapata mkopo wake.
Aidha kufuatia Tangazo la Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia lililotolewa tarehe 17/10/2016 linalohusu uhakiki wa wanafunzi wanaoendela na masomo ya shahada  zoezi litakalofanyika kwa wiki mbili kuanzia tarehe 19/10/2016. TAHLISO inaomba kila mwanafunzi anayesoma shahada kuangalia majina yaliyotolewa kwenye tovuti ya TCU ili kuhakikisha jina lake lipo,na kwa yule ambaye hataona jina lake awasiliane na uongozi wa TCU haraka iwezekanavyo ndani ya wiki hizo mbili kuanzia tarehe tajwa hapo juu  ili kuepuka usumbufu utakaojitokeza.



STANSLAUS PETER KADUGALIZE

MWENYEKITI WA TAHLISO