Saturday, October 22, 2016

Walioshinda tuzo za MTV Mama 2016

 List yote ya walioshinda tuzo za MTV Mama 2016

  1.  Winner Best Group - Sauti Sol wa Kenya  

     2.  Winner Best Pop/Alternative Act - kyle deutsch & shekhinah wa South Africa

     3.  Winner BEST FEMALE - Yemi Alade << Nominees Josey (Ivory Coast) MzVee (GH) Tiwa  (NG) Vanessa (Tanzania)

     4.  Winner BEST International Act - Drake, nominees walikua
Beyonce, Adele, Future and Rihanna.

     5. Winner Best Live Act - Cassper Nyovest 

     6. Legend Award - Hugh Masekela, a South African trumpeter, flugelhornist, cornetist, composer, and singer 

     7. Winner Best Lusophone - C4 Pedro Angola, Nominees NGA, Nelson Freitas, Lizha James and Petro Show.

     8. Winner Best Francophone-Serge (Ivory Coast), Nominees Franko (CMN) J-Rio (GBN) Magasco (CMN) and Toofan

     9. BEST MALE - WIZKID (NG), Nominees AKA (South Africa)
Patoranking (NG) Black Coffee (S.A)
Diamond (TZ)

    10. LISTENER’S CHOICE - Winner Jah Prayzah (Zimbabwe), Tuzo hii ilikua ikiwaniwa na Watanzania Yamoto Band

    11. BEST COLLABO-Dj Maphorsia ft. Wizkid Dj Buckz –Soweto Baby << Afrika mashariki iliwania hii kupitia Sauti Sol ft. Alikiba

    12. VIDEO OF THE YEAR - Winner Nique Ma Vie - Youssoupha (Congo) – Director: Antony Abdelli & Jose Eon

    13. Personality of the year-Caster Semenya << nominees Linda Ikeji, Wizkid, Pearl Thusi, Pierre Aubameyang

    14. Winner Best Group - Sauti Sol Kenya, Tuzo iliwaniwa na R2Bees (Ghana) Toofan (Togo) Navy Kenzo (Tanzania) Mi Casa (S.)

    15. BEST HIPHOP - Emtee (S.A) << ,Nominees Olamide (NG) Kiff No Beat (I.Coast) Ycee (NG)
Ricky Rick (S.A)

    16. BEST NEW ACT - Winner TEKNO (Nigeria) Tuzo hii pia ilikua ikiwaniwa na Rayvanny wa Tanzania ( WCB)

   17. SONG OF THE YEAR - MY WOMAN Patoranking, iliwaniwa pia na 'Unconditionally bae' ya Sauti Sol & Alikiba

  18. ARTIST OF THE YEAR-Wizkid, Nominees Black Coffee (S.A) Diamond (TZ) Sauti Sol (K.E)
Yemi Alade (NG) 

 

Rais Magufuli aiagiza HESLB

Rais Magufuli aiagiza HESLB kuongeza kasi ya ukusanyaji wa madeni.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Magufuli ameagiza Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kutumia Sheria zilizopo kuongeza kasi ya ukusanyaji wa madeni kwa wahitimu walionufaika na mikopo.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akiweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa hosteli za wanachuo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam unajengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA)  kwa gharama ya shilingi bilioni 10.

Amesema kuwa Serikali inadai takribani shilingi trilioni 2.6 kwa wahitimu walionufaika na mikopo ya Elimu ya juu.

“Serikali inawadai wahitimu walionufaika na mikopo ya Elimu ya juu takribani shilingi trillion 2.6 ambazo wanatakiwa kuzirudisha ili ziweze kutolewa kama mikopo kwa wanafunzi wapya na waliopo vyuoni”alifafanua Dkt Magufuli.

Aidha Dkt. Magufuli ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi kusimamia ipasavyo suala la utoaji wa mikopo kwa wanafunzi kwa kuzingatia vigezo vilivyopo kwani lengo la mikopo hiyo inawalenga watoto maskini.

Alisema kuwa kumekuwa na baadhi ya malalamiko ya kuwa  Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inafanya zoezi la ugawaji wa mikopo hiyo kwa upendeleo hivyo kuzitaka uongozi wa Wizara kushughulikia suala hilo.

Mbali na hayo Rais Magufuli amewataka wanufaika wa mikopo hiyo kutimia mikopo hilo kwa malengo mazuri katika kujinufaisha na masuala ya Elimu.

Naye Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof. Joyce Ndalichako  alisema kuwa mradi wa ujenzi wa hosteli hizo utasaidia kuwahudumia wanafunzi 3,840 ambapo unatarajiwa kuisha mwishoni mwa mwezi Desemba 2016.

Katika hatua hiyo Prof. Ndalichako alisema kuwa wanafunzi waliodahuiliwa kwa mwaka huu wapo 58,000 hivyo suala la wanafunzi 66,000 kukosa mikopo hiyo ni upotoshaji unaofanya na baadhi wa watu.

Mradi wa Ujenzi wa Hosteli za wanachuo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wenye majengo 20 kila jengo gorofa nne zenye vyumba 12 unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Desemba mwaka huu.