Saturday, November 5, 2016

Prof.Ndalichako awahakikishia mkopo wanachuo wanaoendelea

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amewahakikishia wanafunzi wanaoendelea na masomo wakinufaika na mkopo kupitia Bodi ya Mkopo wa Elimu ya Juu kuwa hakuna atakayefutiwa mkopo. Profesa Ndalichako aliyasema hayo jana Bungeni mjini Dodoma katika kikao cha Bunge la 11 kinachoendelea. “Serikali haijafuta mkopo kwa mwanafunzi yoyote ambaye anaendelea na masomo yake,” alisema Profesa Ndalichako na kuongeza kuwa kuchelewa kwa mkopo kumetokana na vyuo husika kuchelewa kuwasilisha matokeo ya wanafunzi wanaoendelea kwani hutumika kuwatambua wanafunzi wanaokidhi kigezo cha ufaulu.

No comments:

Post a Comment

KWA MSAADA ZAIDI NITAFUTE KWA SIMU NAMBA.. 0716784460