Wednesday, November 30, 2016

UKIMWI sasa kudhibitiwa

UKIMWI sasa kudhibitiwa kwa njia ya simu

Tanzania imeingia rasmi kwenye mfumo maalum wa kimataifa wa kupata huduma za afya ya UKIMWI kwa njia ya simu bila malipo mfumo ambao umefadhiliwa na nchi ya Marekani.

Akizindua mfumo huo Kaimu Balozi wa Marekani nchini Bi. Virginia Blaser amesema mfumo huo utawafikia zaidi ya watu laki nane huku lengo kuu la mfumo huo likiwa ni kupunguza maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi kutoka asilimia 7.5 mpaka asilimia 5 hadi kufikia asilimia 0.0.

Amesema watu wote ambao wanadhaniwa kuwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi hadi kufikia mwaka 2020 wawe tayari wamepimwa kwa asilimia 90, asilimia 90 waanze kutumia dawa, na asilimia 90 kiwango chao cha maambukizi kiwe kimepungua.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya TAYOA nchini Bw . Peter Masika amesema katika ufadhili wa mfumo huo wao wakiwa ni wasimamizi wa mfumo watahakikisha unawafikia watanzania wote hasa wale wasiofikiwa na huduma muhimu za kiafya na kuwataka watanzania kujitokeza kwa wingi kutumia mfumo huo ili kutokomeza ugonjwa wa Ukimwi.

Chadema: Hatutakubali tena kudhulumiwa 2020

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) ,Vincent Mashinji amesema hawatakubali tena kudhulumiwa kwa namna yoyote  katika uchaguzi wa mwaka 2020.

Dk. Mashinji amesema hayo huku akimtolea mfano wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha, na kuongeza kuwa kuna mambo hutokea bila kutarajia lakini watapambana kwa kila hali,

“Huu ni uchaguzi kuna mtu alitarajia haya yaliyofanywa na Jecha? hii inaonyesha kwenye nchi yetu bado kuna tatizo la utendaji haki, wewe umefanya mara ya kwanza tukanyamaza,ukafanya tena mara ya pili kibabe,tukalalamika, badala ya kutuita tuongee, unasema nendeni mkaseme kokote kule”alisema Mashinji.

Aidha, akiongelea utawala wa Rais Magufuli ,Mashinji amesema kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa utawala bora na matokeo yake yeye ndio amekuwa kila kitu, ameongeza kuwa wakati anaanza  mapambano na rushwa aliamini kwamba angeweza kuliondoa tatizo hilo lakini imekuwa tofauti.

Hata hivyo, Mashinji ameongeza kuwa katika mwaka mmoja wa Rais Magufuli, amesema ameshindwa kusimamia utawala bora baada ya kupiga marufuku mikutano ya hadhara pamoja na shughuli zote za kisiasa nchini kwa kile alichosema kuwa muda wa siasa umekwisha.

Sunday, November 27, 2016

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU KUSOMA "DEGREE" BILA KUPITA "FORM SIX".

Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi Pro.Joyce Ndalichako amepiga marufuku wanafunzi kujiunga na masomo ya Shahada (degree) bila kupita kidato cha sita. Marufuku hiyo itaanza rasmi katika mwaka ujao wa masomo. Prof.Ndalichako emesema mfumo wa elimu huria umechangia kuzalisha wasomi butu kwa kupokea wanafunzi dhaifu kitaaluma.

Ndalichako amesema wanafunzi wanaofeli kidato cha nne na kwenda kusoma certificate na baadae diploma ili wajiunge vyuo vikuu hawataruhusiwa kujiunga na masomo ya shahada (degree) kama hawajarudia (reseat) masomo yao na kupata alama za kwenda kidato cha tano, na wafanye mitihani ya kidato cha sita na kufaulu ndipo wajiunge vyuo vikuu.

Katika utaratibu huo, wanafunzi wa kidato cha nne watakaoruhusiwa kusoma shahada (degree) bila kupita kidato cha 5 na 6 ni wale waliofaulu kidato cha 4 na wakachaguliwa kwenda kusoma katika vyuo vya ufundi daraja la kati (Technicians). Lakini wale wanaokosa "credit" za kuendelea form five na kuamua kwenda certificate mwisho wao utakuwa diploma.

Kuhusu "foundation courses" kwa wanafunzi wa kidato cha sita walioshindwa kupata sifa za kusoma degree, Ndalichako amesema Foundation course haimuongezei mtu sifa.

"Kama mtu amemaliza kidato cha 6 akashindwa kufikisha "points" za kujiunga chuo kikuu, asidahiliwe kwa kusoma foundatiom course. Anapaswa kurudia mtihani wa kidato cha 6 kwa sababu baraza la mitihani linatoa fursa ya kurudia mara nyingi iwezekanavyo. Foundation course haimuongezei mtu sifa kama hana sifa zinazotakiwa kitaaluma" Amesisitiza Ndalichako.


Saturday, November 26, 2016

SIMULIZI

“Kilitokea nini?
Ni swali nililouliza baada ya kuona amenifumba na mimi nilitaka kwenda nae sawa.
“Swali zuri, mwaka 1992 baba yako akiwa anatoka chuo baada ya kumaliza kufanya mitihani, aligongwa na gari lililokuwa linaenda mbio, na dereva kutokomea kusiko julikana, vijana walioliona tukio hilo walijaribu kulifatilia gari lililosababisha ajali na kukimbia bila kufanikiwa, haraka walimpeleka hospital ya mnazi mmoja darajani. Najma alipopata taarifa alizimia, alipozinduka aliomba aende hospital haraka akamuone mumewe kutokana na mapenzi aliyokuwa nayo kwake.
Alipimwa ndani ya siku mbili, ndugu wa Masoud pamoja na Najma waliitwa ofisini kuelezwa kinachoendelea, ndipo waliambiwa anaitaji kuongezewa damu na figo ili kurudisha uhai wake kwani figo moja limekufa na lililobakia halina nguvu za kujitemegea.
Mjukuu wangu! ndugu zake wote waligoma kutoa damu kwa Masoud wakidai wana damu ndogo hata figo pia kumtolea walishindwa, mwanangu akasema bora nife mimi kuliko mume wangu, akaomba apimwe damu kama magroup yanaendana atatoa, na kama figo zake zote zinafanya kazi basi atatoa moja, alisema hivyo huku akiwa anabubujikwa na machozi na ishallah machozi aliyoyamwaga siku hiyo mungu atayalipa tu.
Docta alimuomba aingie kwenye chumba cha maabara, alipimwa damu na kukutwa ana group A kama Masoud na figo zake zote zilikuwa na uwezo wa kufanya kazi vyema, hivyo upasuaji ulianza mara moja wa kutoa figo na damu.
Walifanya upasuaji vizuri, baada ya siku kama tano hivi, Masoud akawa mzima, alimshukuru sana mke wake, walifurahi sana na maisha yakasonga mbele.
Baada ya miezi mitatu, matokeo ya vyuo yalitoka, masoud alipata  maks nzuri, akachaguliwa kuwa miongoni mwa wanafunzi bora wa chuo cha suza, matajiri wenye makampuni makubwa walimuita kwa ajili ya kuongea nae ili awafanyie kazi zao za kiofice, Mungu akamuwekea wepesi na kufanikiwa kujiunga na kampuni moja kubwa tu iko huko mjini.
Ilikuwa ni kama sherehe kwa najma, Hakuamini kama mme wake atapata utajiri wa mali ndani ya miaka michache kiasi hicho, aliinua mikono yake juu mwanangu na kumuombea mmewe kwa mungu ili mali zake ziwe na baraka.
Masoud baada ya kupata kazi kutoka kwenye makampuni yaliyokuwa yanaongozwa na wazungu, alikabidhiwa nyumba na gari la kutembelea, Walitakiwa wahamie mjini yeye na mke wake. ndugu wote waliitana wakaandaa kashuguli kadogo ka kumuombea dua. Alimchukua mkewe pamoja na ndugu zake wengine wakaenda mjini kupaona.
Najma hakuamini kama ipo siku moja angeishi kwenye nyumba ya kifahari haraka hivyo, siku ya kwanza alipofika alizimia zaid ya mara moja kwa sababu ya mshangao, wapo baadhi walimcheka kwa ushamba lakini haikuwa ushamba bali mazingira tu yalimchanganya, tokea kuzaliwa kwake alikuwa hajawai kukanyaga kwenye nyumba yenye mandhari nzuri..
Masiku, wiki, miezi ilikatika baada ya kuamia mjini, shida zote ziliwakimbia na utajiri kupisha hodi, unene ulianza kuiandama mili yao kutokana na kurizika na vyakula wanavyokula, namna walivyokuwa wametakata kwa pesa hukuweza kuwajua kirahisi kama ulipotezana nao miezi mitano au zaid.
Nakumbuka siku moja mwanangu alikuja kunitembea akiwa na gari dogo la kutembelea, tuliongea mengi akanipatia pesa za matumizi, ila katika maongezi yetu nkamwambia “mwanangu, mali hizo ni za mwanaume, siku yoyote anaweza kukuacha na wanaume wa siku hizi wasivyokuwa na haya,  anaweza asikupe chochote japo mali mmechuma wote, hivyo basi kuna kijishamba kinauzwa hapo jirani laki tatu na nusu, inabidi ukinunue kisha uweke watu wajenge japo kijibanda, maisha yanaweza kukushinda huko utakuja uendelee na kwako.
Mwanangu hakuwa mbishi, alinisikiliza ila akanambia sasa hivi hizo pesa hana akipata tu atakuja kulinunua, sasa sijui alisahau! au vipi maana sikumuona tena.
Maisha yao yalisonga mbele, shamba kubwa la masoud lililokuwa huku kijijini, kwa kuwa walikuwa hawaishi tena, nyumba iliyokuwa imejengwa ndani ya shamba iliendelea kuwepo, waliitwa watu wakalima mpunga, na mazao mengine ambayo walihisi badae yatawaingizia faida.
Mjukuu wangu mimi niishie hapo!!, mengine itabidi ukamuulize mama yako nahisi atakuambia, mbane usimpe nafasi japo yanamuuma lakini atakuambia tu kwa kuwa ushaupata mwanzo wake, akikusimlia yeye ni vizuri zaid kwani kuna vya siri nsivyovijua na wewe kwa kuwa unaonekana kuwa tayari una akili anaweza kukuambia, cha mwisho nnachokumbuka mimi, ilikuwa ni usiku wa tareeeeeeeee!  12 mwezi wa 5 mwaka 1993 ambapo tayari alikuwa na mimba yako, alikuja hapa akiwa analia na kijibegi flan hivi kidogo, kumuuliza kulikoni akasema “mama wee acha tu, sikuamini kama masoud anaweza kunifanyia hivi mimi? nliyoyashuhudia kwake yanatosha, na alivyonitesa mimi nkavumilia vyote na mwisho kudai talaka yangu mungu atanilipia tu, kwani nimemvumilia vya kutosha, kiukweli mamaangu bado siamini kama kupata mali tu angebadilika kiasi hiki.
sikuitaji kumuuliza zaid kwa sababu wanaume mi nawajua hasa wakishapata mali, sikumshauri akadai haki yake wala nini, kwa sababu asingeweza kutokana na upole alionao mamaako, nlichomuambia akae chini amuombe mungu wake atamsaidia, wasipolipana hapa duniani basi watalipana kwa mungu.
Ila kwa alichomfanyia kama amefanyiwa kweli mambo aliyoniadisia basi naamini ipo siku moja tu mungu ameipanga kwa kuwa malipo hapa hapa duniani!!, hatta siangaiki najua ipo siku na sisi tutacheka tu kumuona masoud akidhalilika, na kiungo cha mwanangu kilichoko mwilini mwake Nshallah kitamtafuna taratibu!. Alisema bibi.
“Bibi naomba unambie tu kila kitu nadhani mama hatoweza kunambia chochote mimi!
nliongea huku machozi yakinilenga, nlijikuta nkijuta baada ya muda mrefu kumuhisi mama vibaya kumbe alitendewa unyama kwa mujibu wa maneno ya bibi, bibi nae japo macho yalikuwa yakizee lakini yalianza kuiva alipokumbuka mambo yaliyomkuta mwanae, alinigomea kabisa kunambia chochote kilichoendelea, tayari nlishakuwa na mzuka wa kujua kila kitu kilichomtokea mama, sikupoteza muda nlimuaga bibi na kumuambia ntakuja kukusalimia kesho, nlitoka mbio mpaka ndani nkachukua baiskel yangu na kuanza kurudi nyumbani haraka, njia nzima moyoni mwangu kulikuwa na maneno ya” Lazima leo mama anambie ukweli wote sikubali, kumbe baba yangu ndo mshenzi wa tabia hayawani mkubwa!!!.
kama pedeli zingekuwa zinaongea nadhani siku hiyo zingeongea kuwa zinaumia kwa jinsi nlivyo kuwa nazikandamiza. Hazikupita dk kumi tayari nlikuwa nyumbani, nlishuka kwenye baiskel nkaiegesha kwenye mti wa korosho uliokuwa mbele ya nyumba yetu, nliingia ndani kwa kasi nkiita mama, mama tayari alikuwa shambani ikabidi nimfate huko huko.
nlipoingia shambani, nlimkuta anapariria, nkamuita. aligeuka na kunangalia huku akiniitikia.
” Shkamoo
“maraaba mwanangu umerudi baba.
“Ndio nimerudi, mama kuna kitu nataka tuongee ila ndani.
“um we mtoto mbona unavisa hapa haiwezekani kwani?.
“inawezekana ila naomba twende ndani.
“hhmm sawa.
aliniskiliza akanambia nichukue baadhi ya vitu. tulipoingia ndani alikaa kitandani kisha mimi nkavuta kisturi ili kumkalia kitako.
“Mama!, Naomba unisamehe mamaangu kwanza nimekukosea sana, siku zote nlikuwa nahisi uenda ulimtendea ubaya baba ndo maana hutaki kunambia chochote kuhusu yeye, ila bibi kaniambia kila kitu kilichokukuta na kunambia mengine utanambia wewe, nakuomba mamaangu unambie kila kitu kwani kufanya hivyo mimi ntapata msukumo flan wa kunifanya niwe na hasira za kusoma kwa bidii katika masomo yangu ili siku moja niwe na maisha bora, tafadhali mama.
Nlisema. Sikuweza kumuangalia machoni mama.
macho yake yalishabadilika nlipomtamkia maneno hayo, uso wake ulishakaa kihuruma, nlikumbuka maneno ya wahenga ukitaka kumuua nyani usimwangalie usoni, ukimwangalia unaweza kujikuta unashindwa kumuua na kukuua wewe.
“Mwanangu, bibi yako kakuambia kitu gani.?
aliniuliza kwa mshangao, nami nkamjibu.
“amenambia baba alivyokuoa mwaka 1990, mliishi kwa raha, matatizo yalianza alipopata mali, naskia alikutesa sana ndo maana ukarud nyumbani, hakuitaji kunambia vyote kwa sababu hayo mengine kasema hayajui vizuri, naitaji kujua ukweli wote mamaa! please nambie kila kitu mama angu niwe na amani, hata nkiwa natembea niwe najua ukweli wote nnao.
Mama hakuwa na jinsi, baada ya kusikia bibi ashanambia nusu, aliona haina maana tena akaamua kunisimlia kila kitu kilivyokuwa.
” Ni kweli mwanangu, baba yako anaitwa Masoud, ila namchukia kwa yale aliyonifanyia, na sikufundishi hata siku moja umchukie babaako kama utamwona, kwani waswahili wanasema mpende aliemtendea ubaya mtu muhimu katika maisha yako.
Sikuitaji kukuambia chochote kwa sababu ni story inayoniumiza ndani ya moyo wangu kila nkiikumbuka, na najaribu kuisahau moyoni lakini huwa nashindwa.
Babaako alikuwa ni mtu mzuri sana, alikuja kubadilika ghafla baada ya mimba yangu kuanza kukua, na sitomsameehe mpaka kiama kinasimama kwa alichonifanyia….
Mama alianza kulia, huruma iliniingia lakini nlionesha ukakamavu ili niujue ukweli wote hata nsiotakiwa kuujua nliitaji kuujua.
“nadhani bibi yako amekuambia mpaka tulivyohamia mjini. Alisema.
“Ndio mama
“Ok!! ni kweli tulihamia mjini mara tu baba yako alipoajiriwa kwenye kampuni kubwa na kupatiwa nyumba kubwa ya kuishi, nlifurahi sana nkijua ndo mwisho wa matatizo yangu, nliinua mikono juu na kumshukuru Mungu kwa kuniondolea tabu zilizokuwa zimenizunguka. bila kujua mabaya zaid yanakuja mbele yangu. hapo ndipo nlijua kweli ng’ombe wa maskini hazai na watu kama sisi tumezaliwa kwa ajili ya mikosi.
Tulikaa miezi sita kwa furaha huko mjini, hali yangu ilianza kubadilika kila leo bila kujua tatizo ni nini, kutokana na mapenzi aliyokuwa nayo baba yako kwangu alinipeleka hospital haraka kupima vipimo vyote ndipo nkakutwa nna mimba ya mwezi mmoja.
Mme wangu alionekana mwenye furaha, tulikumbatiana mbele ya docta alietupatia majibu hayo, lakini nilishangaa kipindi tunarud nyumbani kwenye gari hakuniongelesha chochote na kila nlipomuongelesha hakujibu.
tulipofika nyumbani ilibidi nimuuliza.
“Tatizo nini mme wangu?
Nliongea kwa huruma na sauti ya chini kwani tayari nlishahisi kuna kitu nimemkosea mme wangu na mimi nlikuwa sipendi nimkosee kwa lolote.
Nlipomuuliza hivyo aliniangalia sana kwa jicho la husda mpaka nliogopa, alionekana kuwa mtu alojawa na hasira, aligeuka akanipa mgongo kisha akanambia ” SIITAJI KUZAA KWA SASA HIVI.”
TUKUTANE SEHEMU YA SITA……

Viongozi Atcl Wapanguliwa

Bodi  ya Wakurugenzi ya Shirika la Ndege nchini (ATCL) imewaondoa katika nyadhifa zao wakurugenzi wote waliopo katika menejimenti na baadhi ya mameneja, baada ya kubainika kuwa na kasoro za kiutendaji na kielimu.

Uamuzi huo, ambao hautamhusisha  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Ladislaus Matindi, ulitolewa katika kikao kilichofanyika Novemba 18, lengo likiwa ni kuboresha muundo wa ATCL, ili kukidhi matakwa ya muda mfupi wakati muundo wa kudumu ukiandaliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Makao Makuu ya shirika hilo, Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL, Mhandisi Emmanuel Korosso, alisema katika kikao hicho bodi iliamua kuwaengua wakurugenzi watano waliokuwa katika idara mbalimbali, ikiwamo ya biashara, ambayo ilikuwa na kaimu.

Mhandisi Korroso alitaja idara nyingine ambazo wakurugenzi wameondolewa  kuwa ni fedha, usalama, ufundi na uendeshaji, ambayo mkurugenzi wake alikuwa anaelekea kustaafu.

“Kwakuwa wakurugenzi wengi walikuwa wanakaimu  nafasi hizo, tumeamua wakurugenzi wanaokaimu warudishwe katika nafasi zao  za chini, ambazo si menejimenti au wahamishiwe katika vituo vya mikoani,” alisema Mhadishi Korosso.

Alisema bodi pia imeagiza  kuondolewa kabisa katika shirika hilo wakurugenzi na mameneja waliothibitishwa ili waweze kupangiwa majukumu mengine yatakayoendana na sifa walizonazo.

Alisema kikao hicho pia kimemuagiza Mtendaji Mkuu kutangaza mara moja nafasi za wakurugenzi na mameneja zilizo wazi kwa kufuata muundo uliopitishwa.

Mbali na hilo, Mhandisi Korosso alisema kwa sasa shirika hilo limeweza kuongeza nidhamu katika mapato na matumizi, jambo ambalo limechangia kuanza kulipa baadhi ya madeni wakati Serikali ikisubiri uhakiki umalizike ili iweze kuyachukua.

“Tumeweza kudhibiti mapato na matumizi vizuri, kumekuwa na ongezeko la mapato ya uzito wa ziada wa mizigo kutokana na usimamizi mzuri, ukusanyaji wa mapato kutoka vituoni na mawakala umeboreshwa sana kutokana na ufuatiliaji wa karibu wa mauzo,” alisema Mhandisi Korosso.

Aliongeza kuwa, bodi pia imetoa ruhusa kwa wafanyakazi na familia zao kupewa tiketi bure mara moja kwa mwaka kama stahiki ya likizo na tiketi yenye punguzo mara moja kwa mwaka.

Kampuni ya ATCL, ambayo awali ilikuwa haina ndege hata moja, ilianza kufanya  kazi za safari za ndege Oktoba 14, mwaka huu, baada ya Serikali kununua ndege mbili mpya aina ya Bombardier Q400.

Monday, November 21, 2016

TCU Public Notice

TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES (TCU)

Public Notice

APPLICANTS WITH EQUIVALENT QUALIFICATIONS
TCU hereby informs applicants with equivalent qualifications whose names appear in the list that they are required to contact TCU not later than Tuesday, 22nd November 2016.

To view the list please click here...

They can contact the Tanzania Commission for Universities through the following numbers;

Landline: +255 (0) 22 2772657

Hotlines: +255 (0) 683 921 928

+255 (0) 675 077 673

Issued by;
Executive Secretary,
Tanzania Commission for Universities.

ORODHA YA MARAIS NCHINI MAREKANI

Obama Speaks

Obama says he may comment as citizen on Trump's presidency

  • 2 hours ago
  •  
  • From the sectionUS & Canada
  •  
  • comments

President Barack Obama and President-elect Donald Trump shake hands following their meeting in the Oval Office of the White House in Washington, Thursday, Nov. 10, 2016.Image copyrightAP
Image captionMr Obama and Mr Trump met at the White House two days after the election


By convention, former presidents tend to leave the political fray and avoid commenting on their successors.
US President Barack Obama has said he may speak out after leaving office if he feels his successor Donald Trump is threatening core American values.
Mr Obama said he would give Mr Trump time to outline his vision but added that, as a private citizen, he might speak out on certain issues.
Mr Trump spent the weekend interviewing candidates for top jobs in his cabinet.
"I want to be respectful of the office and give the president-elect an opportunity to put forward his platform and his arguments without somebody popping off," Mr Obama said at a forum in Lima, Peru.
But, he added, if an issue "goes to core questions about our values and our ideals, and if I think that it's necessary or helpful for me to defend those ideals, then I'll examine it when it comes".
The president described himself as an "American citizen who cares deeply about our country".

Aliyewahi kuwa Mbunge wa Kasulu Mjini(NCCR) na kuhamia ACT-Wazalendo sasa ahamia CCM

Aliyewahi kuwa Mbunge wa Kasulu Mjini(NCCR) na kuhamia ACT-Wazalendo, Moses Machali ahamia CCM

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA WATANZANIA WOTE. ​

Kutoka mezani kwangu Moses Joseph Machali, Tarehe: 21/11/2016

Napenda kuutaarifu umma wa Watanzania kupitia kwenu waandishi wa habari kwamba ni jambo la ajabu na aibu kwa watu makini na wenye kuhitaji mabadiliko ya kweli Kuacha kuunga Mkono juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano chini Uongozi wa Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli bila kusahau utendaji makini wa Waziri Mkuu wake Mhe. Majaliwa Kasim Majaliwa (Mb) pamoja na mawaziri mbalimbali wameonesha kutaka kufuata mwenendo wa Rais Magufuli na Waziri Mkuu wake.

Mimi Moses Joseph Machali niliyefanya sana siasa za Upinzani hapa nchini na niliyepiga kelele na kupinga siasa za kifisadi zilizoitawala nchi hii; niliyepinga pia ufisadi uliokuwa umeitawala serikali huko nyuma kwa nguvu na uwezo wangu wote nikishirikiana na wapinzani wenzangu, ninaamua kujiunga na watu wanaonesha dhamira safi ya kuiendeleza nchi yetu Tanzania. Watu wenye mwelekeo na dhamira ya kuijenga nchi yetu kwa maendeleo enedelevu ni jamii ya akina Magufuli, Kasim Majaliwa, nk.

Mwaka mmoja wa Uongozi wa Rais Magufuli na baadhi ya wasaidizi wake kupitia hatua mbalimbali zilizochukuliwa dhidi ya ufisadi uliokuwa umeigubika nchi yetu, inatosha kabisa kwa mtu yeyote makini kufanya uamuzi wa kumuunga mkono au kutokumuunga mkono Rais Magufuli.

Mimi nimechagua kumuunga Mkono Rais kwa vitendo, kwa sababu ninaposoma Rekodi yangu ya enzi nikiwa Mbunge (Hansard) na kabla ya kuwa mbunge ni kwamba nilipinga mnoo wizi na ufisadi wa kila aina; Nilipinga Matumizi ya fedha serikalini yasiyo ya lazima na yasiyo na tija kwa taifa (Rejeeni hotuba yangu ya Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi, nikiwa Waziri Kivuli wa wizara hiyo ya mwaka 2014/2015 na 2015/2016), vilevile bila kusahau hotuba zangu mbalimbali Bungeni na nje ya Bunge.

Kwa kushirikiana na wapinzania wenzangu enzi hizo tulishauri na kupinga ufisadi wa kila aina, tuliitaka serikali kufanya mambo yenye tija kwa taifa na sasa kila mwenye macho anaona hatua zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya tano. Miradi kama ya Ujenzi wa Reli, Ununuzi wa ndege mbili na mipango ya kununua ndege zaidi kama namna ya kulifufua shirikia la ATCL ni mambo tuliyoyahitaji kuyaona wapinzani; sasa yanafanyika. Wale wenye dhamira ya dhati ya kuona nchi yetu ikipiga hatua, kamwe hatuwezi kubeza mambo hayo bali kuyaunga mkono.

Wale tuliosema na kupiga kelele kwamba Serikali ni dhaifu ktk kuwachukulia hatua watu mbalimbali wenye dhamana serikalini walioonekana kufanya vibaya serikalini ktk nafasi zao, leo tunaona kumekuwepo na kasi nzuri ktk kuwachukulia hatua watu hao. Hata hivyo leo hii upinzani umepiteza mwelekeo kwa sababu unapingana na kile ulichokihubiri nchini.

Agenda ya kupinga ufisadi siyo ya upinzani tena bali ya JPM na CCM yake au yao. Wapinzani wamegeuka kuwa watu wanaokataa yale waliyoyasimamia na kuyahubiri huko nyuma. Hakika huo siyo uungwana bali aina mpya ya ufisadi nchini na usaliti kwa agenda zao.

Kama kweli sisi tumeokuwa wapinzani na tulioonesha kupinga kwa nguvu zote ufisadi ulioiumiza nchi hii tulimaanisha yale tuliyoyahubiri na kuwaaminisha watu basi tunao wajibu wa kuacha tabia ya kuwa vigeugeu kwa mambo tuliyoyaamini na kuyahubiri. Kutofanya hivyo basi ni mwendelezo wa ufisadi kwa maslahi binafsi.

Ni nani asiyeona kwamba serikali ya awamu ya tano inafanyia kazi mambo mengi tuliyoyapigia kelele? Au tunajifanya kutokukubali ukweli unaoishi kwa ule msingi wa upinzani wa Tanzania kwamba Tukimuunga mkono Mtawala kamwe hatutapata kuaminiwa na wapiga kura nchini na hivyo tupinge tu hata kama ni ukweli? Nadhani kinachofanyika ni mwendelezo wa kupinga hata mazuri ili kutafuta fursa ya wapinzani kukubalika kisiasa zaidi hata kwa njia na mbinu haramu kama kawaida ya siasa zilizo zoeleka hapa nchini kwa miaka mingi.

Taifa hili haliwezi kuendelea kwa kuwa na siasa za kutokukubaliana na ukweli unaoishi. Kama dhamira ya kila mtanzania ikiwemo wapinzani ni kuona nchi ina move basi hatuhitaji kuwa watu wa kupingapinga hata yaliyo mema bali kuyaunga mkono yale yaliyo mema bila kujali yanafanywa na nani bali msingi mzuri unapaswa kuwa ukweli kwa kila jambo.

Serikali ya awamu ya tano imeonesha njia ktk mambo mengi na inastahili kuungwa mkono. Safari ni hatua na ninaamini kwamba hata yale yanayoonekana kutokufanyiwa kazi ndani ya mwaka mmoja uliopita na ambayo yalishindikana huko nyuma, bado yanaweza kuja kufanyiwa kazi huko mbeleni. Serikali ya JPM imejitahidi sana tukilinganisha na huko tuliko toka. Uongozi huu unafanana sana na ule wa akina Hayati EDAWARD MORINGE SOKOINE chini ya hayati Baba wa Taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere.

Daima ninaamini ktk yale ninayoyaamini pasipo kufungwa na ukada bali kuangalia ukweli ni upi. Hata kelele wanazopiga baadhi ya watu kwamba maisha yamekuwa magumu kwa sababu ya Magufuli ni propaganda tu kwa sababu hakuna uhusiano wa maisha magumu na suala la KUDHIBITI wapiga dili wa fedha na mali za umma bali tukubali kwamba wapiga dili waliozoea kupiga dili na kuziingiza fedha walizopiga ktk mzunguko kwamba siyo jambo la msingi ktk kujenga uchumi imara.

Uchumi imara hauwezi kujengwa kwa kuruhusu ubadhirifu wa fedha na mali za umma au hata za mtu mmoja mmoja. Kinachoonekana hivi sasa ni kama nchi inasukwa upya na hivyo tuwaunge mkono viongozi wa serikali ya awamu ya tano kwa mema wanayoyafanya na kuwashauri kurekebisha ktk yale ambayo hayajakaa vizuri. Tuachane na siasa nyepesi za kutaka kuona kwamba mazuri ni yale yanayofanywa na wapinzani huku mambo hayohayo yakifanywa na CCM yaonekane hayafai na kutajwa kuwa ni ya hovyo. CCM ya JPM siyo ile ya 2015 kurudi nyuma kidogo. Hii ni tofauti na ninaiunga mkono.

Hivyo basi leo Tarehe 21/11/2016 ninatangaza rasmi kwamba ninajiunga na timu JPM kwa maslahi ya taifa kwa kuwa sioni sababu ya kupingana na yale niliyoyapigania na itakuwa ni sawa na mtu kupigana na kivuli chake mwenyewe. Kwaherini Upinzani nimeamua kuanza siasa mpya za masuala yale niliyoyaamini na ninayoyaamini. Imani ni Matendo Na Matendo ni imani. Piga vita ufisadi kwa imani na Matendo.

Moses Joseph Machali
X-mbunge, Kasulu Mjini 2010-2015,

Sunday, November 20, 2016

Lowassa alionewa CCM

Bashe adai Lowassa alionewa CCM, aeleza uhusiano wao kwa sasa


Mbunge wa Nzega, Hussein Bashe (CCM) amesema kuwa anaamini waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa aliondolewa kwa kuonewa katika mchakato wa kugombea urais ndani ya CCM.

Bashe amesema kuwa kitendo hicho alichokiita cha kiuonevu ni changamoto kubwa ndani ya CCM na kwamba wengi wameonewa katika michakato ya kuwania nafasi mbalimbali.

“Yaliyomkuta Lowassa yamewakuta wengi ndani ya CCM, hivyo jambo hilo sio geni,” Bashe anakaririwa na Mwananchi. “Wapo waliobaki na wapo walioamua kuhama chama kwa sababu ni binadamu. CCM ina historia hiyo, hii ndiyo changamoto yake kubwa,” aliongeza.

Mbunge huyo alifafanua kuwa kwakuwa Lowassa alituhumiwa kwa mengi ndani ya chama hicho, alipaswa kuitwa na kuelezwa tuhuma zake na sababu za kuondolewa jina lake ili umma ufahamu.

Alisema kuwa katika chama hicho, kashfa nyingi hufanywa kwa sababu maalum na hubuniwa kwa ajili ya kufikia lengo fulani dhidi ya mtu au kikundi cha watu.

Alisema kuwa mbali na sakata la Richmond lililopelekea Lowassa kujiuzulu nafasi ya uwaziri mkuu, masakata ya Lugumi na Tegeta Escrow ni sehemu yale yaliyobuniwa kwa lengo maalum.

“Tazama wanavyofunika sakata la Lugumi. Usiende mbali angalia sakata la Escrow. Tumeadhibu waliopata fedha kutoka benki ya Mkombozi, vipi wa Stanbic? Wizi mwingine uliofanywa nchi hii una uhusiano kati ya Serikali na vikundi vya watu wenye uhusiano na Serikali,” Bashe aliliambia Mwananchi.

Akizungumzia uhusiano wake na Lowassa ambaye alikuwa anamuunga mkono wakati wa mchakato wa kugombea urais kupitia CCM, Bashe alisema hivi sasa hawana uhusiano tena wa urafiki wa kisiasa.

Alisema kuwa alimshauri sana Lowassa kutohama CCM, avumilie, lakini hakufanikiwa kumshawishi, hivyo waliagana.

“Lowassa ni mzee wangu. Ni mtu ambaye namheshimu na nitaendelea kufanya hivyo, ingawa kwa sasa hatuna uhusiano wa kisiasa,” alisema.

Lowassa alihama CCM baada ya jina lake kukatwa katika mchakato wa kuwania urais, alihamia Chadema na kupewa nafasi ya kugombea urais katika uchaguzi unaotajwa kuwa na ushindani mkali zaidi tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi.

Akataa Kulipwa Mshahara wa Urais

Donald Trump Akataa Kulipwa Mshahara wa Urais

Rais mteule wa Marekani, bilionea Donald Trump amesema hatakubali kupokea mshahara wa urais pindi atakapokuwa madarakani.

Trump ameweka msimamo huo jana katika mahojiano maalum na mtangazaji maarufu, Lesley Stahl katika kipindi cha 60 Minutes, aliyetaka kufahamu kuhusu uamuzi wake juu ya mshahara wake akiwa ni mfanyabiashara mkubwa.

“Sijawahi kuzungumzia hili, lakini jibu langu ni hapana,” alisema. “Nafikiri inanibidi kupokea kwa mujibu wa sheria $1, kwahiyo ntachukua $1 (Sawa na shilingi 2,200 za Tanzania) kwa mwaka. Lakini hata sijui ni nini,” aliongeza.

Ingawa mtangazaji huyo alimkumbusha Trump kuwa anaiacha $400,000 kwa mwaka, rais huyo mteule alisisitiza, “sitachukua mshahara. Sitapokea.”

Wakati wa kampeni, Trump aliahidi kuwa atajiweka kando na biashara zake endapo atachaguliwa kuwa Rais wa Marekani, na kwamba atajikita zaidi katika kutimiza ahadi zake kwa Wamarekani. Alisema kuwa biashara zake ataziacha mikononi mwa watoto wake.

Wasira Kukata Rufaa tena

Wapambe wa Wasira Kukata Rufaa tena Kupinga Ushindi wa Bulaya

Baada ya Mahakama Kuu, Kanda ya Mwanza kutupilia mbali maombi ya wananchi wanne wa kutaka itengue ushindi wa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Ester Bulaya (Chadema), walalamikaji hao wamesema watakata rufaa katika Mahakama ya Rufaa kwa kile walichosema kuwa Mahakama hiyo haikutenda haki katika kutoa maamuzi hayo.

Novemba 18, mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza iliyokuwa inasikiliza kesi hiyo namba moja ya mwaka huu, katika Mahakama ya Mkoa wa Mara mjini Musoma, chini ya Jaji Noel Chocha, ilitupilia mbali kesi hiyo na kumthibitisha Bulaya kuwa ni Mbunge halali wa jimbo hilo.

Wananchi hao wanne walikuwa wamefungua kesi hiyo wakipinga ushindi wa Bulaya dhidi ya Stephen Wasira kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana.

Baada ya hukumu hiyo kutolewa waandishi wa habari walimhoji mmoja wa walalamikaji Janes Ezekiel, ambaye alisema kuwa watakaa na wenzake waone namna ya kukata rufaa.

Hata hivyo baadaye mlalamikaji mwingine Ascetic Malagila alimwambia mwandishi wa habari hii kuwa tayari wamekubaliana na wenzake pamoja na mwanasheria wao kuwa watakata rufaa katika Mahakama ya Rufaa kupinga hukumu hiyo, kwa kile alichoeleza kuwa wameshindwa kwa sababu ya uonevu na kwamba watatafuta haki yao katika Mahakama ya Rufaa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Wasira alidai kuwa tayari walalamikaji hao pamoja na wakili wao Constantine Mutalemwa, wamekutana na kukubaliana kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa kutafuta haki.

Kabla ya hukumu hiyo kutolewa Jaji Chocha, alirejea baadhi ya vifungu vya sheria pamoja na hoja mbalimbali zilizotolewa na waleta maombi (walalamikaji) na wajibu maombi wa kwanza, wa pili na watatu.

Jaji Chocha alisema kuwa kutokana na kupitia vifungu vyote vya sheria pamoja na ushahidi uliotolewa na waleta maombi katika Mahakama hiyo, ni kwamba ushahidi wao haujajitosheleza katika hatua ya kutengua ubunge wa jimbo hilo.

Alisema kuwa iwapo ataamua kufuta matokeo hayo atawasababishia wananchi wa jimbo hilo ambalo ni miongoni mwa jimbo lenye watu masikini sana kukosa haki yao.

Alisema kuwa madhara ya kurudia uchaguzi ni makubwa sana, sanjari na gharama za uendeshaji wa uchaguzi mpya, ambao utaligharimu taifa na wananchi kwa ujumla kwa sababu gharama za uchaguzi ni sehemu ya kodi ya kila mwananchi.

Akirejea mwenendo mzima wa kesi hiyo tangu ilipofunguliwa katika Mahakama hiyo, Jaji huyo alikiri kutokea kwa kasoro kadhaa katika kipindi cha uchaguzi hadi kutangaza matokeo na kusema kuwa ni kawaida ya uchaguzi wowote kuwa na kasoro ndogondogo na kuongeza kuwa hata nchi zilizoendelea kasoro huwa hazikosekani.

Alisema kuwa katika kesi hiyo kasoro nyingi zilizojitokeza zimeonekana mara baada ya matokeo kutangazwa, lakini katika mchakato mzima wa upigaji kura hakuna kasoro zilizobainishwa, ambazo zingeweza kuonekana kwenye fomu yoyote ya malalamiko anayokuwa nayo msimamizi wa uchaguzi, ambazo zingeonesha kuwa uchaguzi haukuwa wa huru na haki. Alibainisha kuwa si kila kasoro inayojitokeza kwenye uchaguzi inaweza kuathiri matokeo ya uchaguzi.

Hata hivyo alisema kuwa pia msimamizi wa uchaguzi huo Lucy Msoffe alifanya uzembe mkubwa sana wakati alipofika katika hatua ya kuandika idadi ya wapiga kura na kwamba alipaswa kuwa makini kwa kutokuandika takwimu kimakosa.

Akizungumza nje ya Mahakama hiyo wakili wa mjibu maombi Paul Kipeja, alisema maamuzi yaliyotolewa na Mahakama hiyo waliyatarajia tangu mwanzo wa kesi hiyo kwa sababu hakukuwa na hoja zozote za msingi za waleta maombi.

Kuhusu gharama walizotumia katika kesi hiyo wakili Kipeja alisema kuwa watakaa pamoja na wakili Tundu Lissu, ili waweze kurudishiwa gharama zao zote walizotumia kuendeshea kesi hiyo.

Saturday, November 19, 2016

scholarship

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE, TECHNOLOGY AND
VOCATIONAL TRAINING

PUBLIC NOTICE

GRADUATE STUDENTS SCHOLARSHIPS TENABLE IN BRAZIL

1.0 CALL FOR APPLICATION
Applications are invited from qualified Tanzanians for the Graduate Student
Scholarship Program (PEC-PG. The goal of this program is to train students on Post-
Graduate studies in Brazilian higher education institutions. More information about
Scholarships is available at http://dce.mre.gov.br/PEC/PECPG.php

2.0 QUALIFICATIONS
Applicants must:
• Have completed and passed a bachelor / Master Degree and an Acceptance Letter
from a Brazilian Higher Education Institution;
• Be financially responsible for a one-way ticket to Brazil;
• Bear own maintenance expenses for at least 60 days before the start of the PEC-PG
scholarship payments; and
• Have proved proficiency in Portuguese.

3.0 SELECTED CANDIDATES WILL:
• Receive Doctoral Scholarships
• Receive one-way Ticket from Brazil to the Capital of the Country of Origin or
Residence (To be used at the completion of studies)
• Be excepted from Tuition payment or any kind of academic fees
Receive medical/ dental/pharmaceutical care provided by Brazilian State sponsored
health system (SUS)

4.0 MODE OF APPLICATION
Applications can only be made online at http://inscricao.capes.gov.br/individual

5.0 DEADLINE
Deadline for submission of applications is 25th November 2016
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY
Public Notice
The Ministry of Education, Science and Technology, would like to announce to the
general public scholarships opportunities to the qualified Tanzanian Citizens
interested to pursue Masters degree programme in the Kingdom of Thailand for the
academic year 2017-2018.
1.0 How to apply:
Applicants are required to use, International Cooperation Agency (TICA) website
www.tica.thaigov.net which will enable them to obtain application forms and
medical report form
2.0 Area of Priorities
Applicants are required to apply in the fields of Government priorities, such as
Agribusiness, Irrigation, Oil and Gas, Engineering and Management, Health and Allied
Sciences, Science and Technology, Telecommunications, Geology, Petroleum Engineering
and Mining.
3.0 Financial conditions:
The scholarship will cover:
• Round trip air ticket;
• Settlement allowance and a monthly living allowance;
• Accommodation;
• Tuition and supplementary fees;
• Life and health insurance.
4.0 Eligibility
• Applicants must have an undergraduate degree with upper second class or above;
• Applicants should be resident citizens of the United Republic of Tanzania; and
• Candidates should not be more than 40 years of age at the date of application.
5.0 Documents required to be submitted
Candidate should submit their application forms and a copy of the following
documents:
• Birth certificate;
• Three (3) copies of TICA application form affixed with photographs;
• Two (2) letters of recommendation or Referees (from application Academic
advisor or Employer);
• Three (3) Copies of degree certificate in English;
• Three (3 ) copies of transcripts of studies (mark sheets) in English;
• English language certification eg.TOEFL, IELTS, Institute of Foreign Affairs
Test (INFA Test) within 2 years.
6.0 Submission
The dully filled application forms with all required documents must be submitted
at the address below.
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology
Directorate of Higher Education Office Registry
7 Magogoni Street,
P.O. Box 9121,
11479 DAR ES SALAAM.
7.0 Deadline for submission of application forms is 20th December 2016

Pope Francis names 17 new cardinals of Roman Catholic Church

  • 7 hours ago
  •  
  • From the sectionEurope

Media captionAmong those appointed was the Archbishop of Dhaka, Bangladesh - the country has never had a cardinal before

Pope Francis has named 17 new cardinals of the Roman Catholic Church from around the world, many of whom will help choose his successor.
Only cardinals under the age of 80 can vote on the next Pope. Thirteen of those named cardinals on Saturday are under 80, and are now eligible to succeed him.
It is the third time in three years that Pope Francis, the first Latin American Pope, has named new cardinals. He has used each opportunity to promote members from outside the College's traditional European base.

Image copyri
Image captionThe Archbishop of Kuala Lumpur, Anthony Soter Fernandez, is congratulated on being named cardinal

The new cardinals come from countries including the Central African Republic, Bangladesh, Papua New Guinea and Mauritius, among others.
During the ceremony, Pope Francis decried what he said was a "growing animosity" between people, and raised concern over those who "raise walls, build barriers and label people".
"We live at a time in which polarisation and exclusion are burgeoning and considered the only way to resolve conflicts," he said.

Grey line

The new cardinals

Mario Zenari, Italy (who will remain in his role as Papal Nuncio to Syria)
Dieudonne Nzapalainga, Central African Republic
Carlos Osoro Sierra, Spain
Sergio da Rocha, Brazil
Blase J Cupich, USA
Patrick D'Rozario, Bangladesh
Baltazar Enrique Porras Cardozo, Venezuela
Jozef De Kesel, Belgium
Maurice Piat, Mauritius
Kevin Joseph Farrell, USA
Carlos Aguiar Retes, Mexico
John Ribat, Papua New Guinea
Joseph William Tobin, USA
Anthony Soter Fernandez, Malaysia
Renato Corti, Italy
Sebastian Koto Khoarai, Lesotho
Ernest Simoni, Albania